Atabatu Abbasiyya imeanza kujenga msingi katika mradi wa uwanja wa Ummul-Banina (a.s)

Katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya Sayyid Mutwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini, ametangaza kuanza kwa ujenzi wa msingi katika mradi wa uwanja wa Ummul-Banina (a.s).

Katibu mkuu ameviambia vyombo vya Habari kuwa “Tumetembelea mradi wa uwanja wa Ummul-Banina (a.s), mafundi kutoka kitengo cha miradi ya kihandisi wameanza kujenga msingi wenye urefu wa (mita 12)”.

Akaongeza kuwa “Wanafanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya kukamilisha mradi ndani ya muda mfupi, akasisitiza kuwa watajitahidi kununua nyumba zilizopo ndani ya eneo la mradi wa uwanja wa Ummul-Banina (a.s)”.

Mheshimiwa katibu mkuu akaonyesha matumaini makubwa aliyonayo ya kuongeza uwanja utakaotumiwa na mazuwaru kwenye ziara zinazohudhuriwa na mamilioni ya watu na siku za Ijumaa.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: